Jumatatu , 8th Sep , 2014

Rapa mkali kabisa wa muziki wa Dansi Nchini, Mao Santiago baada ya ukimya wa muda mrefu sasa, eNewz imeweza kukutana na kuzungumza naye ambapo ameanika mipango yake ya kurejea na kazi mbili kwa mpigo mwishoni mwa mwezi huu.

Mao Santiago

Mao Santiago aambaye tetesi zimekuwa zikienea mtaani kuwa matumizi ya dawa za kulevya ndiyo yamemuweka kando na muziki amesema kuwa, yeye yupo vizuri tu na kwa sasa anafanya kazi mwenyewe akiwa anatumia nafasi hii kupumzisha kichwa chake kabla ya kurejea tena kwa kishindo katika muziki.

Repa huyu hata hivyo ameweka wazi kuwa, yupo tayari kufanya kazi na Bendi yoyote ambayo itakuwa tayari kufanya naye kazi bila siasa nyingi.