Jumatatu , 25th Jul , 2016

Aliyekuwa meneja wa Poz kwa Poz (PKP) maarufu kwa jina la Mubenga ameongea na Enews na kusema kuwa sasa hafanyi tena kazi na mwanamuziki Ommy Dimpoz pamoja na Nedy na kwamba sasa anaendelea na kazi zake mwenyewe.

Aliyekuwa meneje wa Pozi kwa Poz (PKP) Mubenga

Mubenga amesema “Kwa sasa najipanga ili kuja na kampuni yangu ambayo itaitwa Bengaz Entertainment ambayo itakuwa inahusika na maswala yote ya burudani, hivyo wadau wangu waelewe kwamba kwa sasa sifanyi kazi tena na pozi kwa pozi”.

Hata hivyo Mubenga hakuweka wazi sababu iliyopelekea yeye kuachana na PKP huku akisisitiza kuwa anarudi katika kazi zake alizokuwa akizifanya kabla ya kuungana na pozi kwa pozi.