
Oliver Mtukudzi enzi za uhai wake
Taarifa za kifo cha Mtukuzi zimethibitishwa na record label yake ya Gallo Record Company huku wakishindwa kuweka wazi juu ya ugonjwa ambao umepelekea kifo cha nguli huyo wa muziki.
Wabunge mbalimbali wa Zimbabwe wametoa pole kwa familia na mashabiki wa Mtukudzi huku pia wakimtaka Rais kutangaza msiba wa kitaifa.
"Tumepoteza nembo ya taifa, namwandikia Rais Emmerson Mnangagwa kuomba atangaze msiba wa taifa kwa heshima ya shujaa huyu kwa mchango wake wa kitaifa kwenye sekta ya muziki, sanaa na utamaduni'', amesema Mbunge wa Norton Temba Mliswa.
Moja ya viongozi wengine waliotoa pole ni Waziri wa zamani wa Elimu, Michezo, Sanaa na Utamaduni nchini Zimbabwe David Coltart ambaye amesema "Pumzika kwa amani Oliver Mtukudzi, kama kuna mtu yeyote amewahi kuitangaza Zimbabwe ni wewe. Asante kwa kutufanya tufurahi kwa muda mrefu."
Mtukudzi maarufu kama Tuku alikuwa ni msanii na mwandishi mashuhuri wa ngoma mbalimbali huku akiwa ni moja ya wasanii wenye albam nyingi zaidi akiwa nazo zaidi ya 60.
Mapema mwaka jana alilazwa katika hospitali moja mjini Harare kwa shinikizo la moyo. Hata hivyo aliruhusiwa na hali yake ikaimarika.
RIP #OliverMtukudzi last time I met you and your family was at the NBA Africa Game and what a performance you gave with my mama @YvonneChakaX2 during the Legends Night.
NERIA remains to be my all time favorite from you.
Your legacy lives on. pic.twitter.com/sGQfJeYkP9— Jokate Mwegelo (@jokateM) January 23, 2019