Jumatano , 2nd Mar , 2022

Mchekeshaji maarufu mitandaoni Omary Abeid 'Mzee wa Mjegeje' anasema amempa talaka mke wake na kumrudisha kwao kwa sababu maisha yalikuwa magumu.

Picha ya Mzee wa Mjegeje

"Nilikuwa na mke wangu bahati mbaya maisha yalikuwa magumu, nikaanguka kidogo kifedha nikasema mwanamke sio nyanya wala kitunguu umkatekate umle, ikabidi nimrudishe kwao na nikampa na talaka".

Mzee Mjegeje ameongeza kusema mwanamke huyo alizaa nae mtoto mmoja na sasa hivi ameshaolewa na mwanaume mwingine.