Nikki wa Pilli Kushoto, Kulia ni Nyandu
Nikki amejibu tuhuma hizo za Nyandu kupitia eNewz ya EATV kwa kusema kamwe Weusi hawawezi kuzungumzia maisha ya watu wengine pamoja na yao binafsi kwa sababu siyo malengo ya kundi lao na kuongeza kwamba maisha ya B.O.B hayawahusu hivyo hawawezi kuwaongelea .
"Nyandu ana uhuru wake wa kuzungumza lakini kamwe sisi hatutaweza kuzunguza yanayowahusu wao kwa sababu siyo kazi yetu. Tatizo 'mission' zao hazifanani na za kwetu, 'mission' za Weusi siyo za kuzungumza maisha yetu binafsi kwenye media au ya watu wengine kwa sababu hayatuhusu. Tutazungumza kuhusu muziki wetu,kazi zetu na muziki wetu" - Nikki wa Pili.
Pamoja na hayo Nikki ametangaza hali ya hatari kwa ma rappa waliopo kwenye game juu ya ujio wake mpya unaotegemea kusikika siku chache zijazo kwamba ubunifu, mashahiri pamoja na flow ni vitu ambavyo amejipanga kuwaaletea mashabiki zake.
Nikki amesema anawaonea huruma Mc's wengi kwani amekuja na mtindo tofauti wa mashahiri kitu ambacho kitazidi kumfanya aonekane bora katika game hii ya bongo.
Tazama hapa chini Nikki wa Pili alivyofunguka zaidi.





