Rashida Wanjara
Rashida Wanjara amesema wakati wa Mungu ni wakati sahihi ila ujana na maamuzi ndiyo ulimchelewesha asipate mtoto japo watu walidhani kwamba hataweza kupata mtoto.
Akizungumza na EATV & EA Radio Digital Rashida Wanjara amesema "Wakati wa Mungu ni wakati sahihi, binafsi ujana na maamuzi ndiyo vilinichelewesha kupata, wapo watu walijua kuchelewa kwangu kuzaa kwamba nina matatizo maana nimeitwa Tasa nimeitwa Mgumba, kila mtu alikuwa ananijaji anavyojua yeye ila mwisho wa siku ukweli nilikuwa naujua mimi mwenyewe"
Aidha Rashida Wanjara ameongeza kusema amepata mtoto wa kiume, jina lake ni Shayan ambalo asili yake ni uarabuni na maana yake ni mtu tajiri.