Jumatano , 16th Feb , 2022

Aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi 'Mr II Sugu' amewajibu waliomdhihaki kwenye mtandao wa Instagram kwa kumpa mke wake ujauzito baada ya kumsema kwamba ni mgumba.

Picha ya Mr II Sugu

Sugu amejibu hilo kwenye 'Punchline' ya wimbo wake mpya wa taita aliomshirikisha @billnass ambapo unasema

"Sina waganga kwangu Mungu ndio muumba, kumbuka wadangaji wa Insta waliposema wife wangu mgumba, hatukuwajibu tukawajibu kwa mimba, leo tuna watoto wanagawana vyumba kwenye mjumba".