Jumamosi , 16th Aug , 2014

Msanii wa muziki Young Suma. Amewataka mashabiki wake kufahamu kuwa, katika harakati za kuweka kazi yake katika kiwango kinachostahili, ameamua kusitisha kutoka kwa video yake ya Minister wiki moja zaidi.

Young Suma

Young Suma amesema kuwa, hatua hii imefikiwa baada ya yeye na uongozi wake kukaa na kujadili na kuona kuwa, ni busara kuwatendea haki mashabiki kwa kuirudisha kazi hii jikoni, hatua ambayo sasa inaendelea ili kuifanya ifikie kiwango chake.

Tags: