Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwingira afunguka kummaliza Babu wa Loliondo

Jumatatu , 8th Apr , 2019

Mchungaji wa Kanisa la Efatha Ministry lililopo Jijini Dar es salaam, Josephat Mwingira, amefunguka jinsi alivyommaliza Babu wa Loliondo na kikombe chake, ambacho alidai kuoteshwa na Mungu.

Akizungumza kwenye ibada ya Jumapili ya Aprili 7 2019, Mchungaji Mwingira amesema maombi aliyoyafanya ndiyo yalisababisha kupotea kwa babu wa Loliondo na kikombe chake, kwani alichokuwa akifanya hakikuwa sahihi mbele za Mungu.

Mwingira aendelea kufunguka

Mwingira ameendelea kusema kwamba Mungu hawezi kuzungumza na mtumishi wa Mungu kuhusu kuponya watu kwa miti, kwani Mungu huongea juu ya kunusuru roho za watu, hivyo kama ni kuponya watu kupitia miti, basi ataongea na wataalam wa masuala ya miti ili wafanyie utafiti, ila kwa Mchungaji kutumia miti kuponya ni sawa na uchawi.

“Ikaja ya Loliondo, na yenyewe ikabeba, Mungu haongei na miti, Mungu anaongea na watu, sasa huyu anasema Mungu alinionyesha miti, Mungu akuonyeshe mti badala ya kukuonesha watu!. Mungu hasemi na sisi kuhusu miti, ataongea na madaktari wafanye utafiti kwa miti, sisi tunaongea na roho, miti ya nini!?, pana mgawanyo wa kazi, ukiwa muhubiri anahangaika na miti ni uchawi, na yeye tukamshughulikia”, amesema Mwingira.

Ikumbukwe kuwa mwaka 2011 Mchungaji Mstaafu wa kanisa la Kilutheri Tanzania, Ambilikile Mwasapile, alisema kuwa ameoteshwa na Mungu mti wa kutibu magonjwa mbali mbali ikiwemo Ukimwi, na kukusanya maelfu ya watu alkitibu kwa shilingi 500, huku mamia ya watu wakipoteza maisha wakiwa njiani kwenda nyumbani kwake Loliondo kupata tiba.

Hivi sasa mchungaji huyo haendelei na tiba hiyo, lakini alifanikiwa kukusanya pesa nyingi kutokana na maelfu ya watu waliokwenda, na pia serikali iliweza kupeleka huduma za kijamii kwa haraka katika eneo hilo lililopo mkoa wa Arusha.

Mchungaji Mwingira

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala