Jumanne , 8th Jan , 2019

Binadamu alivyoumbwa na Mungu anapaswa kujisitiri kwa kuvaa mavazi yatakayofunika mwili wake. Lakini mavazi haya hayapaswi kuvaliwa kwa muda wote (masaa 24 kwa siku), kutokana na sababu mbali, za kiafya au za kawaida kama ilivyo asili ya uumbaji.

Nchi zenye ukanda wa hali joto ikiwemo Tanzania, kulala huku ukiwa umevaa nguo ni moja ya vitu hatari kiafya, kwani inaweza kusababisha madhara kiafya.

Hapa nakupa sababu tano muhimu ambazo zitakazokufanya kuanzia leo usilale na nguo yoyote, na hii ni kwa faida yako mwenyewe.

1. Kulala vizuri

Hapa inaeleweka wazi kisayansi kuwa ili ulale vizuri mwili wako unahitaji kutulia, upoe, na ndio maana tunaoga kabla ya kulala, ili kupunguza joto mwilini,  ukiwa umevaa nguo mwili wako unabaki kuwa na joto,  na kukufanya ukose usingizi na kukosa utulivu,  lakini ukilala bila nguo, unaruhusu mwili wako kupata hewa ya kutosha na kusaidia kupoza joto la mwili, na kukupa usingizi mzuri zaidi.

2. Kuacha mwili upumue

Kila sehemu ya mwili wetu umeundwa kwa seli zinazohitaji hewa ili zipumue, ukiwa unalala na nguo zinakuwa hazipati hewa ya kutosha hata kama mwili unakuwa haufanyi kazi yoyote zaidi ya kutulia tu. Hii ni zaidi kwa wanawake ambao wanalala na nguo za ndani , ukilala na nguo za ndani unawapa fursa backeria na aina ya 'yeast' kukua ndani ya mwili. Hivyo kulala bila nguo itakuepusha na magonjwa yatokanayo na bacteria hasa kwa wanawake.

3. Husaidia kuondoa msongo wa mawazo na mwenza wako
   (Stress free with partner)

Wote tunajua kukumbatiana wakati umelala na mwenzi wako ni njia bora ya kuondoa msongo wa mawazo, lakini iwapo utafanya hivyo mukiwa hamjavaa nguoo ni bora zaidi. Unajua kwa nini!?. Hii ni kwa sababu mawasiliano ya ngozi kwa ngozi bila kujihusisha na tendo la ndoa ni bora zaidi na kukufanya akili itulie na kukufanya ujihisi vizuri zaidi, na kuondoa mawazo yote. Pia husaidia kupunguza uwezekanao wa kupata maradhi ya moyo na kukufanya uwe mwenye furaha.

4. Kuwa karibu na mwenzi wako

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa kwa zaidi ya wanandoa 1000 wa nchini Uingereza, ulionesha kwamba wanandoa wanaolala bila nguo wana furaha zaidi kuliko wale wanaolala na nguo. Hii ni kutokana na yale yalioyoelezwa kwenye maelezo ya kipengele chana 3, hivyo inasaidia kukuza uhusiano wao na kuburudishana, kutengeneza 'muunganiko' zaidi kutokana na kulala bila kikwazo chochote kati yao.

5. Kupunguza uzito
Utaona kama ni jambo la ajabu kuwa kulala bila nguo kunahusiana vipi na kupunguza uzito!?. Lakini ukweli ni kwamba ukiwa unalala 'uncomfortable', utakuwa na stress zaidi ambazo zitakusababisha kula vyakula ambavyo havifai kwa afya ya mwili, ili tu ujifurahishe. Lakini ukilala ukiwa umetulia hukupunguzia msongo wa mawazo, na kukufanya uwe usiyekuwa na wasiwasi wa jambo lolote.

Hebu fikiria kuanzia sasa kufuata muongozo huu kwa afya yako ya mwili na kiakili pia.