Kiungo Ally Niyonzima raia wa Rwanda (Kulia) akisaini mkataba wa miaka miwili mbele ya ,Mtendaji Mkuu wa Azam Fc Abdulkarim Amin.
Kupitia mitandao ya kijamii ya Klabu hiyo, imeelezwa kwamba huo ni usajili uliotokana na mapendekezo ya benchi la ufundi chini ya kocha mkuu wake Aristica Cioba.
Niyonzima ambaye yumo kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Rwanda Amavubi anakua mchezaji wa pili kufuatia usajili wa kiungo Awesu Awesu kutoka Kagera Sugar.