
Montreal wamesema Drogba ataungana na wachezaji wenzake kwa mazoezi ya kabla ya kuanza kwa msimu.
Muda mfupi baadaye, mchezaji huyo wa miaka 37 aliandika kwenye Twitter: “Niko safarini kwenda Qatar kujiandaa kwa mwanzo wa msimu.”
Drogba alifanya mazungumzo na Chelsea mwezi Desemba kukiwa na uvumi kwamba huenda atarejea Chelsea kufanya kazi pamoja na wakufunzi.
Wakati huo, Montreal, wanaocheza Ligi Kuu ya Marekani na Canada (MLS) ilikiri kwamba Drogba alikuwa ameelezea nia ya kutaka kuisaidia Chelsea na kwamba hali ilikuwa haimo mikononi mwao tena.
D
Msimu uliopita, Drogba ndiye aliyekuwa mfungaji mabao bora wa Montreal, akiwafungia mabao 11.