Jumanne , 9th Sep , 2025

Rais wa Klabu ya Yanga, Hersi Said, amekiri kuwa ana deni kubwa kwa mashabiki wa klabu hiyo juu ujenzi wa Uwanja. Akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Yanga 2025, Hersi ameeleza kuwa Mchakato wa Uwanja upo safi, na wanasubiri hati kutoka Wizarani.

Eng Hersi Said - Rais wa Klabu ya Yanga

“Najua nina deni kutoka kwa mashabiki na wanachama wa Yanga SC ambalo ni uwanja, Sisi Yanga ombi letu lilikuwa kuongeza upana na sasa tumebakiza mchakato wa kusubiri hati ya kumiliki eneo kwa mradi wa kujenga uwanja wetu." 

''Mchakato wa uwanja upo safi, Mfadhili wetu GSM yupo tayari na tunasubiri hati kutoka Wizarani na siwezi kuondoka Yanga mpaka uwanja ujengwe"- Eng. Hersi Said, Rais wa Yanga.