Jumamosi , 11th Dec , 2021

Mshambuliaji wa zamani wa Barcelona, Inter Milan na timu ya taifa ya Cmaeroon ,Samuel Et'oo amechaguliwa kuwa rais wa shirikisho la Soka nchini Cameroon 'Fecafoot' baada ya kushinda kwenye  uchaguzi wa chama hicho uliofanyika leo

(Mshambuliaji wa zamani wa Cameroon, Samuel Et'oo aliyeshinda urais)

Etoo amempiku mpinzani wake Seidou Mbombo Njoya aliyekuwa anachuana naye baada ya wagombea 5 kujitoa asubuhi ya leo kabla ya Uchaguzi.

Et'oo sasa ataliongoza shirikisho hilo kwa miaka minne ijayo huku akiwa na jukumu la kukiongoza chama hicho huhodhi michuano ya AFCON 2021 yanayotaraji kuanza Januari-Februari 2022.