
Ongala amesema wachezaji wa timu hiyo ni wenye kutaka mafanikio, hivyo wanampa morali ya kufundisha kikosi hicho tofauti na alivyofikiria mwanzoni kutokana na kuzoea maisha ya Dar es Salaam.
Ongala aliwahi kuwa Kocha Msaidizi wa klabu ya Azam FC kwa miaka kadhaa, lakini aliicha klabu hiyo na kwenda nje kwa masomo na kisha kurudi nchini mwaka jana na kujiunga na Maji Maji mwishoni mwa mwaka huo huo.