Jumatano , 19th Aug , 2020

Neymar junior Dos santos huwenda akakosekana katika mchezo wa fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya siku chache zijazo endapo Shirikisho la soka Barani Ulaya (UEFA) watazingatia kanuni zao walizoziweka baada ya janga la Corona kutokea Duniani ya Kutokubadilishana jezi baaada ya mchezo.

Neymar akiwa tumbo wazi huku ameshikilia jezi mkononi aliyobadilishana na mchezaji wa Rb leipzig Marcel Halstenberg baada ya mchezo kati ya PSG na RB Leipzig kumalizika.

Psg ilifuzu fainali ya ligi ya mabigwa kwa mara ya kwanza  katika historia ya klabu hiyo  tangu iliyoanzishwa  mwaka 1970 baada ya kuifunga  timu ya Rb Leipzig ya Germany kwa bao 3-0  na hivyo kumsubiri mshindi kati ya Lyon na Bayern Munich zitakazoumana usiku wa leo.

Baada ya mchezo huo kuisha  nyota wa timu hiyo Neymar alibadilishana jezi na mchezaji wa Rb leipzig  Marcel Halstenberg kama tamaduni za soka kabla ya janga la Corona, kwa kitendo hicho Neymar anatafsirika kukiuka kanuni za kuthibiti janga la COVID-19 ambapo adhabu ni kukosa mchezo moja.

JE PSG ITAATHIRIKA VIPI IWAPO ITAMKOSA NEYMAR?

Kiufundi endapo  Psg watamkosa Neymar katika mchezo wa fainali itawaathiri sana timu hiyo ambayo inacheza kwa ushirikiano mkubwa wa wachezaji watatu  kwenye safu ya ushambuliaji ambaye  ni Neymar  Kylian Mbappe na  Angel di Maria. 

Hivyo wapinzani wanaweza wasiwe na uoga tena  na kujipanga  vizuri kuwathibiti wachezaji waliobaki kiwepesi ukifananisha na siku anazokuwepo Neymar ambayo katika hatua hizi anaonekana kuwa katika kiwango bora cha kiuchezaji.

JE PENGO LA NEYMAR LINAZIBIKA?

Si rahisi kuziba pengo la Neymar Jr kutokana na aina ya wachezaji waliopo mfano Choupo Moting, Pablo Sarabia na Mauro Icardi, kwa hawa aina yao ya uchezaji ni tofauti na mbrazil huyo.

Hivyo kama Kocha Mjerumani  Thomas Tuchel atataka kupata ushindi atalazimika kubadili mbinu zake za kucheza pasipo kufiria kuziba pengo la Neymar ambaye ana kipaji cha kipekee ukilinganisha na hao waliotajwa.