Alhamisi , 1st Aug , 2019

Afisa Habari wa Simba, Haji Manara ameahidi kuachia ngazi kwenye nafasi yake ndani ya klabu hiyo endapo mahasimu wao Yanga watawazidi kwa kujaza uwanja katika mechi zao.

Haji Manara

Ameyasema hayo katika mkutano na wanahabari Jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kadi mpya za wanachama na mashabiki ambazo zitatumia mfumo wa kibenki.

Manara amesema endapo Yanga wataizidi Simba kujza uwanja katika mchezo wake siku ya kilele cha 'Wiki ya Wananchi' Agosti 4 dhidi ya Kariobangi Sharks, basi yuko tayari kuacha kazi ya usemaji wa klabu hiyo.

"Nawasihi mashabiki wetu wanunue tiketi kwa wingi, hatuogopi siku sisi, Al-Ahly kafa Jumanne hapa na watu walifika elfu 60. Naomba muirekodi hii vizuri, ikitokea tumezidiwa idadi ya mashabiki na wenzetu, mimi naacha kazi Simba", amesema Manara.

Aidha Simba imetangaza viingilio katika mchezo huo, ambapo viti vya mzunguko ni Sh. 5,000, VIP B&C ni Sh 15,000, VIP A Sh 30,000, Platinum Sh 100,000 na Platinum Plus Sh 150,000.

Mtazame hapa akizungumza zaidi.