Pamoja na Ronaldo kuwahi kunukuliwa akisema huenda watakuwa marafiki huko mbeleni, lakini Messi amesema hawana ukaribu hivyo ni ngumu wao kuwa marafiki.
"Sijui kama tutakuja kuwa marafiki, maana urafiki unajengwa kupitia kukaa pamoja na kujuana lakini sisi hatuna hiyo nafasi '', amesema.
Aidha messi amesema wachezaji hao hawana tofauti kila kitu kipo sawa ila maisha yao hayaingiliani sana kila mtu ana mambo yake na mara nyingi wanaonana kwenye sherehe za tuzo na kwenye michezo ya El Clasco tu.
Msimu huu Messi amefunga mabao 20 pamoja na kutoa pasi za mwisho 10 kwenye La Liga na Ronaldo amefunga mabao 11 na kusaidia mengine manne.