Jumanne , 2nd Nov , 2021

Mshambuliaji wa Barcelona, Sergio Aguero anatazamiwa kuwa nje ya uwanja kwa muda wa miezi mitatu baada ya kukutwa na tatizo katika mishipa yake ya moyo jambo linalopelekea  wakati mwingine apumue kwa tabu.

(Sergio Aguero akitolewa uwanjani baada ya kupewa huduma ya kwanza)

Taraifa ya Aguero kutakiwa kuwa nje ya uwanja imekuja baada ya daktari anayemtibia kwasasa Dkt. Josep Brugada kuthibitisha kuwa nyota huyo anapaswa kuendelea kupata matibabu chini ya uangalizi maalum.

Aguero alipata tabu ya kupumua alipokuwa uwanjani wakati Barcelona ilipokuwa inacheza na Derpotivo Alaves kwenye La Liga Jumamosi ya Oktoba 30, 2021 jambo lililomfanya ashindwe kuendelea na mchezo na kutolewa dakika 41