Kikosi cha Simba kitaondoka nchini Jumamos kwenda Angola kucheza mchezo wa klabu bingwa dhidi ya Primeiro de Agosto
Kwa mujibu wa ratiba yao ya maandalizi Ahmedi amesema kikosi kinaingia kambi leo Jumanne tayari kwa maandalizi ya mchezo dhidi ya de Agosto, na ameweka wazi kuwa kikosi kitaondoka nchini siku ya Jumamosi Oktoba 8 siku moja kabla ya mchezo, na baada ya mchezo kumalizika siku ya jumapili wataanza safari ya kurejea nyumbani.
Wakati kikosi hicho kikiwa kinaanza maandalizi hayo wataendelea kuwakosa wachezaji watatu Jimmyson Mwanuke, Shomari Kapombe na Peter Banda hawa wote wana majeruhi. Simba wanaelekea kwenye mchezo huu wakiwa wametoka kushinda mchezo wa Ligi kuu NBC Premier League dhidi ya Dodoma Jiji kwa mabao 3-0 na sasa wanaongoza Ligi.