
(Kocha wa Spurs, Antonio Conte)
Siku ya jumatano klabu ya Spurs ilitangaza kuhairishwa kwa mchezo wake dhidi ya Rennes kutokana na kuwepo kwa maambukizi 13 ya Uviko 19 kwenye timu yao huku klabu ya Rennes wakipinga vikali wakiita ulikuwa ni uamuzi binafsi kuliko wa pamoja,
"Uefa kwa kushirikiana na vilabu vyote viwili tumejitahidi kupata suluhu ya kuupanga upya kwenye kalenda mchezo huu lakini juhudi zote tulizozifanya hazijaweza kupata suluhu iliyokubaliwa na vilabu vyote, matokeo yake mchezo hautoweza kurudiwa kuchezwa” UEFA wamesema.
Tayari Rennes wamefuzu kwenda hatua ya 16 bora huku klabu ya Vitesse wakikamata nafasi ya pili baada ya kumfunga klabu ya NS Mura huku Spurs wakishika nafasi ya tatu.
Mchezo huu ambao ulipangwa kuchezwa Dec 31, sasa maamuzi ya mchezo huo yataamuliwa na kamati ya maadili na nidhamu ya UEFA wiki ijayo.
Wachezaji nane wa Spurs walikutwa na maambukizi ya Uviko 19 huku sheria za UEFA zikisema kama kuna wachezaji 13 wapo vizuri kiafya na golikipa akiwepo basi mchezo unapaswa kuchezwa .