Kocha wa Twiga Stars, Bakari Shime akitoa maelekezo kwa wachezaji wake akiwa benchini.
Kuelekea kwenye mchezo huo, Kocha wa Twiga Stars, Bakari Shime amesema wachezaji wapo vizuri na wamejiandaa vizuri na mchezo huo ukizingatia wanagahamu vizuri wapinzani wao.
"Namshukuru Mungu tupo salama, tumefanya maandalizi leo na wachezaji wana ari kubwa ya mchezo huo" Alisema Shime.
Twiga Stars ipo kundi B na timu za Zimbabwe, Botswana na Sudan kusini huku ikitaraji kushuka tena dimbani Oktoba 2, 2021 kucheza na Botswana kabla ya kucheza na Sudan Kusini.





