(Ferland Mendy na Casemiro wa Real Madrid)
Nyota hao watakosekana kutokana na kuoneshwa kadi mbili za njano hivyo kutumikia adhabu ya kukosa mchezo mmoja huku kiungo mkabaji Federico Valverde na beki wa kushoto Mkongwe Marcelo wakitazamiwa kuchukua nafasi zao
Real Madrid ina kibarua kigumu cha kupindua meza kwani walifungwa bao moja kwa sifuri kwenye mchezo wao wa mkondo wa kwanza nchini Ufaransa kwa bao la Kylian Mbappe ambapo inaelezwa huenda akawafiti kucheza mchezo huo.
Naye matajiri wa jiji la Manchester, Manchester City watakuwa wenyeji wa Sporting Lisbon ya Ureno huku akiwa na faida ya ushindi wa mabao 5-0 kwenye mchezo wao wa mkondo wa kwanza.




.jpg?itok=5cvL0YaP)
