Jumatano , 10th Mei , 2023

Wawakilishi pekee wa Tanzania kimataifa, klabu ya Yanga Jumatano ya Leo Mei 10, 2023 imeibuka na ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Marumo Gallants ya Afrika Kusini kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza wa nusu fainali ya kombel la Shirikisho barani Afrika.

Magoli ya Yanga SC yamefungwa na kiungo wake mshambuliaji Stephan Aziz Ki dakika 64 na la pili limefungwa na winga Bernard Morrison dakika 90+2 ambaye alitokea benchi kuchukua nafasi ya winga Tuisila Kisinda.

Ushindi huo unawapa faida Yanga SC kuichungulia fainali ya michuano hiyo kuelekea mchezo wao wa marudiano dhidi ya Marumo Gallants unaotaraji kuchezwa Mei 17, 2023 nchini Afrika Kusini ambapo ili Marumo ifuzu fainali inahitaji kushindi utofauti wa magoli 3.