Jumatano , 4th Mei , 2016

Moto mkubwa wa nyika umelazimisha kuhama watu 60,000 kutoka mji wa Fort McMurray ambao ni idadi yote ya wakazi wa mji huo wa nchini Canada.

Moto mkubwa wa nyika umelazimisha kuhama watu 60,000 kutoka mji wa Fort McMurray ambao ni idadi yote ya wakazi wa mji huo wa nchini Canada.

Ndimi za moto zimeteketeza nyumba kadhaa, na kushusha majivu kwenye mitaa katika mji huo uliopo kwenye mkoa wa Alberta.

Wakazi wanaokimbia mji huo wamesababisha foleni kubwa katika barabara kuu inayotoka kwenye mji huo uliopo kilomita 380 kaskazini mwa Edmonton.