Jumapili , 5th Jun , 2022

Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana (MB), amewashukuru wakazi wa jiji la Arusha kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan za kuinua Sekta ya Utalii nchini kwa kuitangaza kupitia Filamu ya The Royal Tour.

Dkt. Chana ameyasema hayo Jijini Arusha aliposhiriki ibada katika kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini Kati, Usharika wa Arusha Mjini. 

Amesema mkoa wa Arusha umebarikiwa na Mungu kwa kuwa na vivutio vingi vya Utalii hivyo wananchi wanatakiwa wazilinde baraka hizo za vivutio kwa kuvitunza.

Akitoa salamu kwa niaba ya waumini wa kanisa hilo Mchungaji Kiongozi  Rachel Axwe  amemwomba  Waziri Chana kumfikishia salamu Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya ya kuitangaza Tanzania kupitia Sekta ya Utalii na kuhamasisha uwekezaji  hali inayowanemeesha pia wakazi wa jiji la Arusha ambao kwa asilimia kubwa wanategemea Biashara ya Utalii.

Waziri Chana yupo jijini Arusha kwa ziara ya Kikazi.