Jumamosi , 11th Feb , 2023

Maandalizi yanaendelea nchini New Zealand kutokana na kimbunga kikali kinachotishia kuyakumba maeneo ya nchi hiyo ambayo tayari yameharibiwa na mafuriko mabaya.

 

Kimbunga Gabrielle kinatarajiwa kukipiga kisiwa cha Kaskazini mwa nchi hiyo kuanzia leo usiku m na kinaweza kuleta upepo mkali na mvua kubwa zaidi.

Wakazi wametakiwa kuhakikisha wanapata mahitaji ya  kutosha kudumu kwa siku tatu iwapo watakwama nyumbani.

Kimbunga hicho kinajiri wiki kadhaa baada ya mvua kubwa kunyesha katika mji wa Auckland.

 Makazi ya kuwahamisha watu yameanzishwa huku  shirika la ndege la taifa, limefuta safari kadhaa za ndani kabla ya kuwasili kwa kimbunga hicho.