
Mkurugenzi wa Makumbusho ya Louvre Laurence des Cars amethibitisha jana Jumatano Oktoba 22 uamuzi wa kujiuzulu kufuatia wizi wa kustaajabisha wa vito kutoka kwa jumba la makumbusho lililo katikati ya jiji la Paris.
Wizi huo ulifanywa baada ya wezi kuchukua dakika saba pekee kuingia kupitia dirishani na kuiba vito vya thamani na kutoroka, wizi ambao Mkurugenzi huyo ameuelezea kama ni kushindwa vibaya kutokana na kuwa na ukosefu wa kamera za usalama katika jumba hilo.
Waziri wa Utamaduni wa Ufaransa Rachida Dati amekataa kujiuzulu kwa des Cars ambaye ameamua kuchukua uamuzi huo baada ya kukagua na kutathmini matokeo ya aliyoyaita kuwa ni ya shambulio baya, tathmini aliyoifanya yeye na Dati na Waziri wa Mambo ya Ndani Laurent Nunez siku ya Jumapili.
des Cars, Mkurugenzi wa jumba la makumbusho kubwa zaidi ulimwenguni ameshikilia uamuzi huo wa kujiuzulu akisema kwamba katika maisha yake ya muda mrefu, hajawahi kuamini kwamba watu wanamiliki kazi zao.
Matamshi yake yamekuja siku tatu baada ya wizi wa kihistoria kufanyika katika ukumbi wa Louvre, ambapo vito vya thamani ya takriban Euro milioni 88 sawa na dola milioni 102 takribani shilingi bilioni 248,864,000,000 viliibiwa.
Msako wa kuwapata wahalifu na nyara nyara walizochukua bado unaendelea. Jumba la makumbusho la Louvre limefunguliwa tena jana Jumatano asubuhi baada ya kufungwa kabisa kufuatia wizi huo Jumba la sanaa la Apollo, ambako tukio hilo la uvunjifu lilitokea, likiwa bado limefungwa kwa sasa.