Mhudumu wa lodge anyongwa na mteja
Gema Haule aliyekuwa mhudumu wa nyumba ya kulala wageni iitwayo Peace lodge, iliyopo Kata ya Matarawe Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, amekutwa ameuawa kwa kukabwa shingoni na kamba ya kiatu na mtu asiyefahamika jina, ambaye alikuwa mteja katika chumba ambacho alipanga kwa siku tano.

