Fahamu kilichojiri katika kesi ya Erick Kabendera
Kesi ya uhujumu uchumi namba 75 ya mwaka 2019, inayomkabili Mwandishi wa Habari za Uchunguzi, Erick Kabendera, imesogezwa mbele hadi Februari 10, 2020, kwa madai ya kuwa upelelezi bado haujakamilika na kwamba mtuhumiwa bado anafanya majadiliano na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini.