Waziri Ummy atoa taarifa kuhusu Covid 19
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ametoa taarifa kuhusu tetesi za uwepo wa mlipuko mpya wa Covid 19 Tanzania ambapo amewataka Wananchi waondoe hofu na kusema Wizara ya Afya inachakata taarifa zilizokusanywa kutoka Hospitali/Vituo mbalimbali ndani ya wiki hii kisha watatoa taarifa.