
Aidha Waziri Ummy amesema “Kwa taarifa za Wagonjwa waliopimwa virusi vya Covid-19 wiki ya kuanzia May 6 - 12, 2023, Watu 6 kati ya 288 walithibitishwa kuwa na corona ikiwa ni pungufu ikilinganishwa na wiki ya April 29 hadi May 05,2023, hakuna kifo chochote kilichothibitishwa kusababishwa na Covid-19”
“Wizara ya Afya inaendelea kufuatilia kwa karibu kwenye Hospitali mbalimbali na tutawapa taarifa kamili, nawaomba Wananchi muendelee kuzingatia kanuni za afya na usafi”