Auawa akituhumiwa kusafirisha mirungi
Martin Kinasa mkazi wa mtaa wa Dkt Mohamed Shein, Kata ya Igoma jijini Mwanza, ameuawa kwa kupigwa kisha kuchomwa moto wakati akijaribu kuwatoroka watu waliokuwa wakimkimbiza kwa kutumia bodaboda kwa tuhuma za kwamba anasafirisha dawa za kulevya aina ya mirungi.