Kijana wa miaka 27 abaka mtoto
Mtoto wa miaka tisa anayesoma darasa la 4 katika moja ya shule za msingi zilizopo Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi, amebakwa mara kadhaa na kijana anayefahamika kwa jina moja la Seif (27), huku akimrubuni kuiba pesa kwa mama yake na kumpelekea yeye.