Rais wa Sri Lanka aomba msaada wa mafuta Urusi
Rais wa Sri Lanka Gotabaya Rajapaksa ameandika katika ukurasa wake wa Twitter kwamba amemuomba Vladimir Putin wa Urusi kulisaidia taifa lake lenye uhaba wa mafuta, kwa kuwa linakabiliwa na mgogoro mbaya zaidi wa kiuchumi tangu Sri Lanka ilipopata uhuru kutoka kwa Uingereza mwaka 1948.