Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bei mpya za mafuta kuanzia leo baadhi ya Mikoa

Wednesday , 6th Feb , 2019

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), imetangaza bei mpya za mafuta ambazo zimepungua ikilinganishwa na mwezi uliopita.

Picha ya gari likijaza mafuta Sheli.

Taarifa iliyotolewa na kaimu mkurugenzi wa Ewura, Nzinyangwa Mchany inasema bei hizo mpya zitaanza kutumika kuanzia leo Jumatano Februari 6, 2019.

Inaeleza kuwa bei za jumla na rejareja kwa mafuta yaliyoingizwa nchini Tanzania kupitia Bandari ya Dar es Salaam, zimepungua kwa viwango tofauti. Inaonyesha kuwa wateja wa rejareja watapata unafuu wa shilingi 175 kwa lita ya petroli wakati wale wa dizeli wakishushiwa kwa shilingi 144 na mafuta ya taa shilingi 156.

Hata kwa bei za jumla, petroli imepungua kwa shilingi 174.03 kwa lita, dizeli kwa shilingi 143.65 na mafuta ya taa shilingi 155.32 na kueleza kuwa kupungua kwa bei hizo kunatokana na kuendelea kushuka kwa bei katika soko la dunia.

Licha ya mabadiliko hayo ya bei, mikoa ya kaskazini itabaki kama mwezi uliopita kutokana na kuwapo kwa shehena iliyopokelewa Januari, 2019 kupitia Bandari ya Tanga huku kukiwa bado kuna akiba kubwa iliyoingizwa Desemba 2018.

Inafafanua kuwa bei za mafuta kwa mikoa ya kusini zilikokotolewa kulingana na gharama za mafuta yaliyopokelewa katika Bandari ya Dar es salaam lakini wiki ya pili ya Januari Bandari ya Mtwara ilipokea shehena ya petroli hivyo kubadili ukokotozi.

Kuanzia Januari 25, 2019 bei ya rejareja ya petroli na dizeli katika mikoa hiyo zilikokotolewa kwa gharama za Bandari ya Mtwara hivyo zitaendelea kubaki kama zilizvyo kuanzia tarehe hiyo.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa