Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Idadi ya wabunge wa upinzani waliojiunga na CCM

Wednesday , 14th Nov , 2018

Ikiwa imesalia siku moja kabla ya kufungwa kwa dirisha la kupokelewa na kupewa dhamana ya uwakilishi kupitia tiketi ya CCM kwa wabunge na madiwani kutoka vyama vingine, mpaka sasa ni wabunge tisa pekee ndio wamejiuzulu.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole.

Wabunge hao waliojiuzulu nafasi hiyo na wengine kufanikiwa kutetea nafasi zao kwa mara nyingine kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), saba kati yao ni kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) huku wawili wakitokea Chama cha Wananchi (CUF).

Wabunge hao kutoka CHADEMA ni; Mwita Waitara (Ukonga), Julius Kalanga (Monduli), Chacha Marwa Ryoba (Serengeti),Godwin Moleli (Siha), James Ole Millya (Simanjiro), Pauline Gekul (Babati) na Joseph Mkundi (Ukerewe) huku upande wa CUF ni Maulid Mtulia (Kinondoni) na Zuberi Kachauka (Liwale . 

Chaguzi hizo za marudio zilipelekea upinzani kususia kuendelea kushiriki mara baada ya kupoteza majimbo yao mfululizo, ambapo CHADEMA kupitia mwenyekiti wake wa chama, Freeman Mbowe kilitangaza kujiondoa rasmi kushiriki chaguzi ndogo zote zilizotangazwa kufanyika na chaguzi zozote zitakazofuata zinazosimamiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa madai kwamba tume hiyo inafanya kazi kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi.

Na baadaye CCM, kupitia kikao cha kamati kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa Chama hicho kilichokaa Oktoba 30, kilitangaza tarehe 15 Novemba kuwa ndio tarehe ya mwisho kwa Chama hicho kuwapokea maombi ya wenye nia ya kujiunga na Chama hicho na kupewa dhamana ya uwakilishi kupitia tiketi ya CCM kwa wabunge na madiwani kutoka vyama vingine.

Na kuongeza kuwa baada ya tarehe hiyo hakuna kiongozi yeyote atakayepewa nafasi ya kugombea uwakilishi wa Chama hicho katika uchaguzi wa marudio badala yake watakuwa wanachama wa kawaida

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja