
Afisa Habari wa Simba, Haji Manara.
Manara amesema hayo ikiwa yamebaki masaa machache ili timu hizo kuweza kukutana katika uwanja wa Taifa ikiwa ni mchezo wa marudiano.
"Ujinga wakati wa kwenda tu,wakati wa kurudi hata wajishike Ugoko lililoandikwa litakuwa tu Insha'Allah. Kufa au kupona", Manara.
Ujumbe huo wa Manara umekuja kufuatia wachezaji wa Nkana Red Devils kuingia uwanjani wakiwa wamjishika kichwani kila mmoja ishara ya kujikuna hivyo Manara amesema kwa hapa hata wakishika ugoko watawafunga tu.
Mchezo wa kwanza wa Simba na Nkana uliochezwa Kitwe, Zambia ulimalizika kwa wekundu wa msimbazi kukubali kupokea kipigo cha mabao 2-1.