
Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, akiupokea Mwenge wa Uhuru ulipowasili mkoani Mbeya Oktoba tatu mwaka jana.
Akizungumza katika makabidhiano ya mbio hizo katika kijiji cha Mkutano Wilayani Momba, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro amesema katika miradi hiyo, 39 itawekewa mawe ya msingi na 17 itazinduliwa na kukabidhiwa kwa walengwa.
Miradi hiyo ni pamoja na Zahanati, Ofisi za kata, Nyumba za Waalimu pamoja na vyumba vya maabara katika shule za Sekondari.