Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Niko tayari kufukuzwa CCM - Elibariki Kingu

Sunday , 19th Mar , 2017

Mbunge wa Singida Magharibi Elibariki Kingu ameibuka na kuweka wazi kuwa yuko tayari kufukuzwa ndani ya chama chake cha CCM kwa kupinga uhalali wa elimu ya Mkuu wa Mkoa wa dar es Salaam.

Katika taarifa yake aliyoitoa leo, Kingu amesema anasikitishwa na ukimya uliotanda miongo mwa wanachama wa CCM kwa hofu ya kufukuzwa uanachama na kuacha Rais Magufuli akisemwa vibaya kila kona ya nchi kwa sababu ya kiongozi mmoja ambaye elimu uhalali wa elimu yake unatiliwa shaka.

"Najua hofu mliyonayo watanzania juu ya huyu RC. Ikiwa mamlaka zitaendelea kufumbia macho. Mimi Elibariki Immanuel Kingu mbunge wa CCM nitakuwa wa kwanza kufukuzwa CCM kama kupinga matendo maovu ya RC huyu itaonekana ni usaliti kwa nchi. Haiwezekani Rais wetu atukanwe kila kona kwa matendo ya mtu huyu. Wana CCM ukimya wetu kwenye hili halikubaliki". Amesema Kingu.

Kingu ambaye amezungumza na EATV kwa njia ya simu na kuthibitisha taarifa, ameongeza kuwa anakerwa na kusikitishwa na kelele zinazoendelea mitandaoni kuhusu tuhuma za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kughushi vyeti vyake vya taaluma huku matusi na kejeli zikipelekwa kwa Rais, na bado wana CCM wako kimya.

Pia ameonesha kukerwa na kile alichokiita matendo yanayokiuka utawala wa sheria yanayofanywa na mkuu huyo wa mkoa.

"Naomba sasa niweke kumbukumbu sawa najua mnamchafua kila anayempinga RC huyu kwa matendo yake ambayo yanakiuka utawala bora. Naomba niwe wa kwanza kufukuzwa CCM kwa kumpinga RC Makonda"
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya