Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

RC Mbeya aagiza wanakijiji kukamatwa

Thursday , 16th Aug , 2018

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, likiongozwa na Kamanda, Ulrich Matei  linawasaka watu wanaodaiwa kufanya uharibifu wa miundombinu ya maji katika Kijiji cha Ngole, Kata ya Ilungu wilayani Mbeya.

Kamanda wa Polisi jijini Mbeya, Ulrich Matei.

Hatua inakuja ikiwa ni siku moja imepita baada ya Mkuu wa Mkoa huo, Albert Chalamila,  kutoa agizo kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Paul Ntinika, kuwa wakamatwe wanakijiji wote kutokana na uharibifu wa miundombinu ya mradi wa maji.

Inadaiwa kuwa uharibifu uliofanywa  katika Kijiji cha Mashesye ni kukata mabomba yaliyokuwa yametandazwa kuanzia kwenye chanzo cha maji.

Kutokana na agizo hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na msako mkali huko katika kijiji cha Ngole kuhakikisha wale wote waliohusika na uharibifu huo wanakamatwa na kufikishwa Mahakamani kwa kosa la uhujumu uchumi.

Mwenyekiti wa Kijiji  cha Mashesye ambacho kiliharibiwa miundombinu ya maji,  Lazaro Mwakalila, amedai kuwa wananchi  wa  Kijiji cha Ngole wakiwa na Mwenyekiti wao walifika eneo lake na kukata mabomba ya maji na kubomoa tanki la maji wakitumia vifaa mbalimbali yakiwamo majembe na mapanga.

Agizo hilo linakuja ikiwa ni siku chache tangu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi, Selemani Jafo kukemea tabia ya baadhi ya Wakuu wa Wilaya kutumia vibaya mamlaka waliyonayo kuwaweka watu ndani.

Jafo alisema hayo jijini Dodoma kwenye kikao kazi na wakuu wa Wilaya 27 walioteuliwa hivi karibuni kilicholenga kuwapa maelekezo ya kazi, ambapo Jafo alisema, tabia hiyo inasababisha wananchi kuichukia serikali, hivyo ameagiza Wakuu wa Wilaya kutumia sheria hiyo kama ilivyokusudiwa na siyo kwa kuonea watu.

Msikilize hapo chini Kamanda, Ulrich Matei ameeleza zaidi kuhusiana na tukio hilo.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja