Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Serikali inakiri kumshambulia Lissu" Mdee

Sunday , 17th Feb , 2019

Baada ya kusambaa mitandaoni kwa sauti inayodaiwa kuwa ni ya Naibu Waziri, Mwita Waitara kuhusu kutovumiliwa kwa msaliti, Mbunge wa Kawe Halima Mdee amesema kwamba kauli hiyo inaonyesha serikali imekiri kuhusika na shambulio la Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Antiphas Lissu.

Mbunge wa Kawe, Halima Mdee

Mdee amechapicha ujumbe huo kwenye ukurasa wae Twitter baada ya kuenea kwa sauti hiyo ambayo imekosoa vikali ziara za nchi za ulaya na Marekani zinazofanywa na Mbunge Tundu Lissu ambaye alishambuliwa kwa risasi Septemba 07, 2017 nje ya nyumbani kwake Jijini Dodoma.

Sauti hiyo inasema kwamba, "mnapokuwa kwenye mapambano, hasa vita vya uchumi, ili nchi itoke ianze kujitegemea, tupange mambo yetu wenyewe sasa yeye anataka turudi tulipokuwa. Kwenye vita kama mkiwa mstari wa mbele halafu mwenzenu anawakwamisha mnamuwaisha yeye. Huu ni utaratibu wa mapambano".

Imeendelea kusema, "kama ukiwa mzalendo ukipotea gharama itatumika kukutafuta lakini kamwe siyo kumtafuta msaliti".

Baada ya kauli hiyo Mdee amesema kwamba, "damu ya mtu haijawahi kumuacha mtu salama...Naona serikali inakiri kuhusika na shambulio la kutaka kumuua tundu lissu..na kwamba mipango ya kutaka kumuua bado inaendelea".

Mbali na Mdee, Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche ameeleza kwamba Watanzania hawatakubaliana na matukio yanayopangwa kudhuru viongozi wa vyama vya upinzani.

"Hizi kauli za kiitarahamwe na za kipuuzi zinazotolewa kuhusu kudhuru viongozi wa upinzani haziwezi kupuuzwa. Kwa yeyote anaepanga majaribio haya ajue wanachama na Watanzania hawatakubali upumbavu huu. Upinzani upo kwa sheria haiwezekani watu wanatishia wenzao kuwaondoa duniani".

Hata hivyo harakati za kumtafuta Naibu Waziri, Waitara kufafanua kauli zake ziligonga mwamba baada ya simu yake ya mkoni kutopatikana.

Sikiliza sauti hiyo hapa chini

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero