Thursday , 3rd Nov , 2016

Rapa anayewakilisha vizuri mkoa wa Mbeya Ice Boy amesema haoni na wala hajapata faida yeyote kwa yeye kufanana na Rapa Tupac mbali na kupewa sifa kuwa amefanana na mwanamuziki huyo.

Ice Boy

 

Akiongea na eNewz Ice Boy amesema anavyoamini yeye ni ngumu sana Tanzania kupata mafanikio kupitia kufanana na Tupac kwa kuwa wananchi na wadau wa sanaa Tanzania hawaitambui faida ya mtu yeyote maarufu hata kama ni staa mkubwa.

 Ice amesema ni bora kutengeneza 'brand' yake ili hata ikitokea siku akipata nafasi ya kutoka nje iwe rahisi  kutumia hiyo nafasi ya kujitangaza kuhusiana na kufananishwa na Tupac huenda kukamuongezea kitu katika maisha yake lakini kwa sasa anaimba anavyopenda kwani hata akimuiga mwanamuziki huyo hawezi kuongeza mashabiki katika muziki wake.