Friday , 28th Oct , 2016

Imebainika kuwa kuzorota kwa biashara ya hoteli katika jiji la Arusha licha ya sababu nyingine pia linatokana na baadhi ya waajiri kutotaka kuwekeza kwa wafanyakazi wao katika kuwapa elimu ili kuweza kuhimili ushindani wa utoaji wa huduma bora mahote

Mkurugenzi Mtendaji wa Progress Center Bi Rose Urio.

 

Mkurugenzi wa Progress Center Bi Rose Urio amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha akisisitiza kuwa muitikio duni kwa washiriki bado ni jambo linaloonesha dhahiri kuwa wamiliki bado wanahitaji elimu zaidi katika uwekezaji huo.

Bi. Urio amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuimarisha sekta hiyo ambayo inaenda sambamba na utalii ili kuongeza pato kwa wamiliki wa hoteli lakini pia kuongeza pato la taifa kupitia kodi

Kwa upande wake mmoja wa mameneja wa Hotel Mkoani humo Neema Gervas amesema umuhimu wa mafunzo hayo ni pamoja na kuwawezesha kutoa huduma bora ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.