Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Vyama 15 vya upinzani vyaungana

Sunday , 9th Dec , 2018

Vyama vya upinzani 15 nchini vimeungana kupinga muswada wa marekebisho ya sheria ya vyama vya siasa ambao ulisomwa kwa mara ya kwanza bungeni mwezi uliopita wakati wa mkutano wa 13 wa Bunge.

Baadhi ya viongozi wa vyama vilivyoshiriki kutoa tamko la pamoja

Vyama vilivyoshiriki katika kutoa tamko la pamoja kupinga muswada huo ni CHADEMA, CUF, DP, ACT Wazalendo, NLD, ADC, CCK, UPDP, Chauma, NCCR Mageuzi vikiongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha Umma (Chauma), Hashim Rungwe.

Akisoma tamko la pamoja katika mkutano huo, Mwenyekiti wa muungano huo, Hashim Rungwe amesema kuwa wameamua kuichagua siku ya leo ya Uhuru kwakuwa ni siku muhimu ya kukumbukwa kwa nchi japokuwa haijasheherekewa kama ilivyozoeleka.

"Tumeitumia siku ya leo ya Uhuru kutoa tamko hili kwani ni siku muhimu kwa taifa letu na serikali ya awamu ya tano kuendelea kufuta sherehe za Uhuru ambazo Duniani kote ni siku ambayo taifa husheherekea kuzaliwa kwake, " amesema.

Kuhusu msimamo wa umoja huo kwenye sheria hiyo wanayoipinga, Hashim Rungwe ameesema hawatokubali kurudi nyuma katika kupigania haki yao hasa katika suala hili kwani wameona dalili za wazi za kutaka kupokonywa demokrasia yao waliyokuwa nayo.

Tumeona nchi nyingi zimeingia katika vurugu kutokana na wao kudai haki zao kwa nguvu ila sisi hatutaki kufanya hivyo ndiyo maana tumeamua kuudai Uhuru huu kabla hatujapokwa na kuliingiza taifa katika matatizo".

"Tunatoa wito kwa watanzania wote bila kujali rangi, kabila na itikadi zao watuunge mkono katika kuzuia sheria hii kandamizi ili kuzuia vurugu kubwa zinazoweza kutokea siku za usoni," ameongeza.

Pia Rungwe ametaja sababu za kuipinga muswada huo kuwa ni pamoja na kutokuwepo kwa uhuru wa kujiamulia na kutoshirikishwa kikamilifu katika mchakato wa kuandaa muswada huo.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa January Makamba

Ziara ya Rais Samia Korea kuanza rasmi Mei 31 2024

Bw. Nazar Nicholas (katikati) akikabiziwa tuzo ya WSIS 2024

Tanzania yashinda Tuzo WSIS 2024, nchini Uswisi

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20