Wednesday , 27th Apr , 2016

Zaidi ya hekari 1,000 za mazao ya chakula zimesombwa na maji, nyumba 10 zikianguka na nyingine zaidi ya 100 zimezingirwa maji katika kijiji cha Changalawe Kata ya Masanze wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro kufuatia mafuriko yaliyosababishwa na mvua.

Mbunge wa jimbo la Mikumi Mhe.Joseph Haule

East Africa Redio imeshuhudi mashamba na nyumba hizo zikiwa zimeanguka kabisa na nyingine kubomoka huku waathirika wa mafuriko hayo wakiomba msaada waharaka ikiwemo chakula, hifadhi ya muda pamoja na mbegu za mahindi za muda mfupi ili wapande upya ili kuwaepusha na baa la njaa.

Nao viongozi wa Serikali ya Kijiji na Kata wameomba msaada wa dharula kuwasaidia wananchi hao huku wakieleza sababu ya mafuriko hayo ni kutokana na Mto Miyombo kubadili uelekeo na kumwaga maji kwenye makazi na mashamba ya wananchi na kwamba jitihada za kurudisha tuta la Mto huo zinahitajika ili kuzuia maafa kwa wananchi.

Mbunge wa Jimbo la Mikumi Mhe.Joseph Haule amefika katika kijiji hicho ambapo amesema anafanya jitihada za haraka kuhakikisha wananchi wanapata msaada wa hifadhi ya muda, chakula pamoja na mbegu na kuhusu tuta amesema kazi hiyo itaanza mapema mvua zitakapopunga.

Sauti ya Mbunge wa jimbo la Mikumi Mhe. Joseph Haule akizungumzia uhutaji wa msaada kwa wananchi wake.