Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wananchi wauwa mamba 300 kulipiza kisasi

Monday , 16th Jul , 2018

Kikundi cha watu wapatao 100 wenye hasira kali nchini Indonesia kimeua mamba takribani 300 baada ya mamba mmoja kujeruhi na kumuua mfugaji aliyekuwa akitafuta malisho.

Mamba waliouwawa na wananchi nchini indonesia

Tukio hilo limetokea katika jimbo la Papua ambapo, Sagito (48) alitumbukia katika bwawa linalotunza mamba hao wakati akitafuta majani ya kulisha mifugo yake.

Kikundi hicho cha watu pamoja na majirani walikasirishwa na uwepo wa bwawa hilo karibu na makazi ya watu ndipo walipoelekea kituo cha Polisi kutoa taarifa lakini licha ya mmiliki wa bwawa kukubali kulipa fidia, wananchi hao hawakukubaliana na uamuzi na kuamua kuwauwa mamba hao.

Mamlaka ya Polisi nchini humo imekiri kutokea kwa tukio hilo na kwamba ipo katika uchunguzi baada ya kukamilika itafungua mashitaka kwa wahusika wa mauwaji hayo.

Matukio ya mamba kuuwa raia yanakithiri nchini humo, mwezi Machi maafisa wa wanyama walifanikiwa kumuuwa kwa risasi mamba mwenye urefu wa mita sita ambaye alimla mfanyakazi mmoja wa shamba la michikichi.

Miaka miwili iliyopita pia mtalii mmoja raia wa Urusi alivamiwa na mamba katika kisiwa maarufu cha watalii kuogelea cha Raja Ampat nchini humo.

HABARI ZAIDI

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP