Wednesday , 9th May , 2018

Msanii chipukizi wa muziki wa kizazi kipya amewachana wanawake wa Dar, akisema kwamba wapo kwa ajili ya kuchezewa na sio kuolewa

Rucky Bebi ameandika ujumbe huo kwenye ukurasa wake wa instagram baada ya kumpongeza mtangzaji wa kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, Jr , na kusema kwamba wanawake wa Dar wamemaliza wanaume wote hivyo sio wa kuolewa.

“Hongera mwanangu, nimeamini Dar es salaam wanawake wa kuchezewa, mwanamke mmoja kamaliza Dar nzima nani ataoa chawote? kujenga familia wapo nje ya dar, amkeni kugawa kama pipi”, ameandika Rucky Bebi.

Hivi karibuni mtangazaji huyo amefunga ndoa ya kimya kimya na mchumba wake wa muda mrefu mkoani Tanga.

Alichokiandika Rucky Beby instagram