Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Harmorapa hana pesa ya kunilipa - Juma Nature

Tuesday , 28th Mar , 2017

Mkongwe wa bongo fleva Juma Kassim Nature 'Sir Nature' amekanusha vikali kulipwa na msanii Harmorapa katika wimbo wa 'Kiboko ya mabishoo' na kudai kwamba kijana huyo hana pesa za kumlipa na kusisitiza yeye alifanya kwa upendo tu.

Nature, Harmorapa

Akizungumza na eNewz ya EATV, Nature amesema kwamba alikubali kushiriki katika wimbo huo kwa sababu anaamini msanii huyo chipukizi ana uwezo mkubwa ikiwa ni pamoja na kuamini atafika mbali.

"Nikisema nimemlipisha Harmorapa pesa kwa ajili ya kolabo nitakuwa nakosea, mimi ni mtu mzima nilikubali kufanya wimbo na msanii yule kwa sababu ni mkali na anajua muziki pia na imani atafika mbali, hawezi kunilipa mimi, ana hela gani" - Juma Nature.

Katika hatua nyingine Nature kutoka TMK amesema yeye ameshakuwa mkongwe hivyo vijana kama kina Harmorapa wanapotokea kwenye ‘game’ inamlazimu kutoa sapoti ili hata watakapoondoka kuwe na watu wa kuendeleza muziki.

Aidha Nature amekanusha kusikia taarifa ambazo Harmorapa alidai kuwa amemlipa Nature kwa kolabo na kuongeza hizo taarifa kwa upande wake hazimkufikia rasmi.

Hata hivyo Harmorapa aliwahi kunukuliwa akisema siyo busara kwa wasanii wakongwe kuwalipisha pesa wasanii wachanga kwa kuwa ndiyo kwanza wanaanza kutafuta pa kutokea na kuweka wazi kuwa kwa upande wake alilazimika kumnunulia nguo Nature za kufanyia video ya ‘Kiboko ya Mabishoo’.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa January Makamba

Ziara ya Rais Samia Korea kuanza rasmi Mei 31 2024

Bw. Nazar Nicholas (katikati) akikabiziwa tuzo ya WSIS 2024

Tanzania yashinda Tuzo WSIS 2024, nchini Uswisi

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20