Tuesday , 18th Mar , 2014

Rapa Abbas Kubaff, kutoka nchini Kenya ameibuka na malalamiko makubwa dhidi ya mamlaka ya hakimiliki ya kazi za muziki nchini humo, Music Copyright Society of Kenya, ambapo ameitaka mamlaka hii kufanya kazi kwa uwazi na haki zaidi.

Abbas ametaja mambo muhimu ambayo mamlaka hii inatakiwa kushughulikia kurekebisha, ikiwepo wasanii kuitwa katika vikao katika hatua za mwisho, njia za kuwasiliana na wasanii kuimarishwa, na pia kutokupendelea lebo moja dhidi ya nyingine kati ya mambo mengine.

Abbas kutokana na malalamiko haya, ameandaa waraka ambao atatumia kukusanya saini za wadau na wasanii watakaomuunga mkono ili kuwezesha kusukuma mambo haya ya msingi kushughulikiwa na kuwekwa katika mstari.